Kamishia
wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Salome
Kaganda akiwaapisha Manaibu Kamishina wa Jeshi la Polisi (DCP)
Modestus Gasper Lyimo na Juma Yussuf (hawapo pichani) leo Jijini Dar es
Salaam. Manaibu Kamishina hao awakupata fursa ya kula kiapo hicho pamoja
na wenzao mnamo tarehe 16 Julai 2016.
MTATURU: JESHI LA POLISI HALIPASWI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA
Mwenyekiti
wa Kamati ya Ulinzi na usalama Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu
akizungumza na askari wa Jeshi la polisi mara baada ya ziara yake katika
makao makuu ya Wilaya hiyo eneo la Ikungi.MFUKO KICHOCHEO WA SAGCOT WASAINI MAKUBALIANO NA SHIRIKA LA BOTHAR KUTOKA NCHINI IRELAND
Katibu
Mtendaji wa Mfuko Kichocheo wa SAGCO Bwa. John J. Kyaruzi akisaini
makubaliano hayo na Mwasisi wa Shirika la Bothar Bw. Peter Ireton huku
wakishuhudiwa na Dkt. Bernard Muyeya (kulia) Mkurugenzi wa Huduma za Nje
ya Nchi wa Bothar na Bwa. Abdallah S. Msambachi ( kushoto) Mratibu wa
Biashara wa Mfuko wa SAGCOT.
Ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa kuongeza tija na uzalishaji kwa
wafugaji wa ng’ombe wa maziwa mkoani Njombe, Iringa na Mbeya, Mfuko
Kichocheo wa SAGCOT yaani SAGCOT CATALYTIC TRUST FUND tarehe 12 Agosti 2016 umesaini makubaliano na Shirika la Bothar kutoka nchini Ireland
ambalo linajihusisha na kutoa misaada mbalimbali inayolenga kutoa fursa
kwa familia zenye kipato cha chini kuweza kuboresha maisha yao kupitia
uwekezaji wa shughuli zinazowaletea kipato hususani kaya zinazojishughulisha na ufugaji.
wafugaji wa ng’ombe wa maziwa mkoani Njombe, Iringa na Mbeya, Mfuko
Kichocheo wa SAGCOT yaani SAGCOT CATALYTIC TRUST FUND tarehe 12 Agosti 2016 umesaini makubaliano na Shirika la Bothar kutoka nchini Ireland
ambalo linajihusisha na kutoa misaada mbalimbali inayolenga kutoa fursa
kwa familia zenye kipato cha chini kuweza kuboresha maisha yao kupitia
uwekezaji wa shughuli zinazowaletea kipato hususani kaya zinazojishughulisha na ufugaji.
Katika
makubaliano hayo jumla ya Ng’ombe wa kisasa 630 wanatarajiwa kuingizwa
nchini katika kipindi cha miaka mitatu. Ng’ombe hao watagawiwa kwa
wafugaji walioandaliwa chini ya miradi inayotekelezwa na Mfuko huo,
Aidha wafugaji watahakikishiwa masoko pamoja na huduma mbalimbali za
mifugo kupitia wataaalamu wa Halmashauri husika.
WAZIRI NAPE AFUNGA MASHINDANO YA GOFU YA WAZI YA TANZANIA JIJINI ARUSHA,WAKENYA WATAMBA
TANAPA,NGORONGORO NA IDARA YA WANYAMAPORI SASA KWENDA KIJESHI
Gwaride
la wahitimu wa mafunzo ya kijeshi kwa askari na maafisa wa Hifadhi za
Taifa likiingia katika viwanja vya mazoezi katika kambi ya mafunzo ya
Mlele wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi
akipokea salamu ya utii kutoka kwa askari wa Shirika la Hifadhi za Taifa
(TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (hawapo
pichani) wakati wa ufungaji mafunzo kwa askari na maafisa hao
yaliyofanyika katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi
akikagua gwaride wakati wa kufunga mafunzo kwa askari wa Shirika la
Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
yaliyofanyika katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi
Askari
na Maafisa wa Hifadhi wakipita kwa heshima mbele ya mgeni rasmi kwa
mwendo wa pole na haraka wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kijeshi
waliyopata katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni
sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya
Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu kutoka mfumo wa
kiraia.ALI KIBA LADY JAY DEE WAFUNIKA TAMASHA LA SEREBUKA 2016 LILILOANDALIWA NA KAMPUNI YA STARTIMES
Msanii, Snura Mushi, akitumbuiza kwenye tamasha hilo.
Msanii, Juma Kassim ‘Juma Nature, akitumbuiza kwenye tamasha hilo.
Msanii Stamina akipagawisha kwenye tamasha hilo.
Wananchi
wakifuatilia Tamasha la Serebula Festival la kuazimisha miaka miwili ya
chanel ya startimes Swahili iliyoandaliwa na kampuni ya Bluelines kwa
kushirikiana na uwawei jijini Dare s Salaam jana
TAARIFA RASMI KUHUSU KIFO CHA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA PILI MZEE ABOUD JUMBE MWINYI
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akitoa taarifa rasmi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuhusu kifo
cha Rais Mstaafu wa Zanzibar wa awamu ya pili Mzee Aboud Jumbe Mwinyi
kilichotokea leo Mji Mwema Dar es Salaam na kuzikwa kesho katika viwanja
vya nyumbani kwake Migombani Unguja.[Picha na Ikulu.]15/08/2016.
Kwa masikitiko makubwa, naomba kuwaarifu kuwa, leo tarehe 14 Agosti 2016, Mzee wetu Alhaj Aboud Jumbe Mwinyi amefariki dunia. Kama mnavyofahamu, Marehemu Mzee Aboud Jumbe ni Rais Mstaafu wa Zanzibar awamu ya pili, ambaye vile vile alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Marehemu Mzee Aboud Jumbe amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu kutokana na umri wake.
Msiba huu umetokea nyumbani kwake Mji Mwema, Dar es salaam. Maziko ya marehemu yatafanyika kesho tarehe 15 Agosti 2016 saa 7.00 mchana ambapo maiti yake itasaliwa katika Masjid Mshawar, Mwembeshauri na kuzikwa nyumbani kwake Migombani.
Kufuatia mchango na juhudi mkubwa ambazo marehemu Mheshimiwa Aboud Jumbe Mwinyi alizichukua katika uhai wake kwa kuitumikia, kuiongoza na kuijenga Zanzibar pamoja na nafasi yake katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nchi yetu imekabiliwa na msiba mkubwa kwa kifo cha kiongozi huyu mahiri.
Kutokana na msiba huu mkubwa kwa nchi yetu, natangaza rasmi siku saba za maombolezo, kuanzia kesho tarehe 15 Agosti 2016. Katika kipindi hicho chote bendera zote zitapepea nusu mlingoti. Kadhalika utaratibu wa maziko utafuata wasia ambao mwenyewe marehemu aliutoa wakati wa uhai wake.
Tunaungana na wanafamilia wote katika kipindi hiki kigumu cha msiba. Naomba kutumia nafasi hii kutoa mkono wa pole kwa wafiwa wote. Tunamuomba Mwenyezi Mungu amjaalie kauli thabit marehemu mzee wetu na amlaze pahala pema peponi, Amin
Kwa masikitiko makubwa, naomba kuwaarifu kuwa, leo tarehe 14 Agosti 2016, Mzee wetu Alhaj Aboud Jumbe Mwinyi amefariki dunia. Kama mnavyofahamu, Marehemu Mzee Aboud Jumbe ni Rais Mstaafu wa Zanzibar awamu ya pili, ambaye vile vile alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Marehemu Mzee Aboud Jumbe amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu kutokana na umri wake.
Msiba huu umetokea nyumbani kwake Mji Mwema, Dar es salaam. Maziko ya marehemu yatafanyika kesho tarehe 15 Agosti 2016 saa 7.00 mchana ambapo maiti yake itasaliwa katika Masjid Mshawar, Mwembeshauri na kuzikwa nyumbani kwake Migombani.
Kufuatia mchango na juhudi mkubwa ambazo marehemu Mheshimiwa Aboud Jumbe Mwinyi alizichukua katika uhai wake kwa kuitumikia, kuiongoza na kuijenga Zanzibar pamoja na nafasi yake katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nchi yetu imekabiliwa na msiba mkubwa kwa kifo cha kiongozi huyu mahiri.
Kutokana na msiba huu mkubwa kwa nchi yetu, natangaza rasmi siku saba za maombolezo, kuanzia kesho tarehe 15 Agosti 2016. Katika kipindi hicho chote bendera zote zitapepea nusu mlingoti. Kadhalika utaratibu wa maziko utafuata wasia ambao mwenyewe marehemu aliutoa wakati wa uhai wake.
Tunaungana na wanafamilia wote katika kipindi hiki kigumu cha msiba. Naomba kutumia nafasi hii kutoa mkono wa pole kwa wafiwa wote. Tunamuomba Mwenyezi Mungu amjaalie kauli thabit marehemu mzee wetu na amlaze pahala pema peponi, Amin
ZLATAN IBRAHIMOVIC AJITAMBULISHA KWA GOLI WAKATI MAN UTD IKISHINDA
Zlatan
Ibrahimovic amefunga goli katika mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya
Uingereza wakati Manchester United ikiibuka na ushindi wa magoli 3-1
dhidi ya Bournemouth na kumpatia kocha wao mpya Jose Morinho ushindi
wa kwanza.
Katika
mchezo huo Juan Mata alikuwa wa kwanza kuifungia Manchester United
katika dakika ya 40 kufuatia makosa yaliyofanywa na mabeki wa
Bournemouth, ambapo baadaye katika dakika ya 59 Wayne Rooney alifunga
la pili kwa mpira wa kichwa.
Juan Mata akifunga goli la kwanza la Manchester United baada ya mabeki kufanya uzembe




















0 Comments